Yanga, Bodi ya Ligi waachana njia panda!

Licha ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) kutangaza tarehe mpya ya kuchezwa mechi ya marudiano kati ya Yanga na Simba, hali ya sintofahamu imeendelea kutanda upande wa Jangwani kuhusu hatma ya mchezo huo wa Kariakoo Dabi.